visitors

display number of visitors

Blog Archive

Theme images by Storman. Powered by Blogger.

Thursday, December 8, 2016

Mtandao mkuu wa kuuza viungo vya wanadamu Misri wavunjwa


Misri imevunja mtandao mkubwa ambao umekuwa ukifanya magendo ya viungo vya wanadamu katika nchi mbali mbali duniani.
Hayo yamefichuliwa na Wizara ya Afya ya nchi hiyo na kubainisha kuwa, watu 45 wanaohusishwa na mtandao huo wamekamatwa, wakiwemo madaktari, wauguzi, mawakala na wanunuzi wa viungo hivyo.
Habari zaidi zinasema kuwa, miongoni mwa madaktari waliokamatwa wamekuwa wakihudumu katika taasisi mashuhuri za afya nchini humo na wengine ni wahadhiri katika vyuo vikuu vya Cairo na Ainu Shams, taasisi mbili kuu za masomo ya juu nchini humo. Aidha mamilioni ya dola za Marekani zimepatikana katika vituo vya afya vya kibinafsi ambapo biashara hiyo haramu imekuwa ikifanyika. Baadhi ya hospitali na zahanati hizo zimesajiliwa na serikali ijapokuwa aghalabu yake hazijaidhinishwa na Wizara ya Afya.



0 on: " Mtandao mkuu wa kuuza viungo vya wanadamu Misri wavunjwa "