Mkurugenzi wa Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu nchini Tanzania (NIMR), Dkt Mwele Malecela, ambaye alitangaza kugunduliwa kwa virusi vya Zika nchini Tanzania, amefutwa kazi.
Taarifa kutoka kwa mkurugenzi wa mawasiliano ya ikulu Gerson Msigwa inasema Rais wa John Magufuli ametengua uteuzi wa mkurugenzi huyo mkuu.
Taarifa hiyo hata hivyo haijaeleza sababu ya kufutwa kazi kwa Dkt Malecela, siku moja tu baada yake kutangaza kwamba kuna virusi hiyo.
Hata hivyo, kulikuwa kumetokea habari za kukinzana kutoka kwake na wizara ya afya kuhusu kuwepo kwa virusi vya Zika nchini Tanzania.
Alitangaza kuwepo kwa virusi hivyo nchini Tanzania siku ya Alhamisi lakini Ijumaa, baada ya habari hizo kuenea kwenye vyombo vya habari, waziri wa afya Ummy Mwalimu akatoa taarifa kukanusha habari hizo.
- Njia 10 za kujikinga dhidi ya virusi vya Zika
- Dkt Malecela akithibitisha kupatikana kwa Zika Tanzania
"Uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa NIMR atakayejaza nafasi iliyoachwa na Dkt Mwele Malecela utatangazwa baadaye," taarifa hiyo inasema.
Dkt Mwele Malecela alikuwa ametangaza kwamba virusi hivyo vimepatikana mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania na Mkoani Geita, kaskazini magharibi mwa Tanzania.
Kwa mujibu wake, virusi hivyo viligunduliwa wakati wa utafiti uliofanyika kutokana na uhalisia kuwa kuna mazingira yanayowezesha kuzaliana kwa mbu wanaoeneza virusi hivyo.
Chanzo BBC Swahili
0 on: " Malecela, Afisa mkuu wa NIMR aliyetangaza kuna Zika Tanzania afutwa kazi "