Fainali ya awamu ya kumi ya Kombe la Mataifa ya Afrika miongoni mwa kina dada, imerudia matokea yake ya awamu ya tisa iliyochezwa nchini Namibia, ambapo Nigeria iliichapa Cameroon mabao 2-0.
Mechi ya fainali inatarajiwa kuchezwa katika uwanja wa Ahamadou Ahidjo, mjini Yaounde huku rais Paul Biya akitarajiwa kuwa miongoni mwa mashabiki wengi watakaohudhuria mechi hiyo.
Kina dada kutoka Nigeria Super Falcons wanatarajia kulitetea taji lao kwa kupata ushindi wa mara ya nane kati ya mechi 10 walizoshiriki.
Timu ya Cameroon ya Indomitable Lionesses wanatafuta kupata ushindi kwa mara ya kwanza katika kombe la Taifa, mechi ambayo itakuwa mechi yao ya fainali ya tatu.
Timu hizo mbili zilipitia ushindani mkali katika nusu fainali walipotoka na ushindi mwembamba wa bao 1-0.
Cameroon inatarajiwa kupata goli moja katika shindano hilo, huku Nigeria wamefunga magoli 12.
0 on: " Fainali:Kina dada wa Cameroon kukutana na Nigeria "