visitors

display number of visitors

Blog Archive

Theme images by Storman. Powered by Blogger.

Monday, November 28, 2016

Raisi Magufuli atuma salamu za rambirambi kwa raisi wa Cuba Raul Catsro kufuatia kifo cha Fidel Castro


Rais wa Tanzania John Magufuli amemtumia salamu za rambirambi rais wa Cuba Raul 
Catsro kufuatia kifo cha rais mstaafu wa Cuba Fidel Castro. Katika salamu hizo magufuli 
amesema kuwa amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Fidel Castro. Katika taarifa kwa vyombo vya habari Magufuli amesema

kuwa kwa niaba yake pamoja na wananchi wa taifa la tanzania ametoa pole kwa wananchi wa Cuba kwa kumpoteza mtu muhimu. Amemsifu Fidel

kwa kuwa kiongozi sahupavu ambaye atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika ukombozi wa nchini za Kusini mwa Afrika pamoja na misaada mikubwa aliyotoa kuboresha huduma zas kijamii kwa wananchi.


''Alikuwa rafiki wa Tanzania na Afrika nzima,historia ya Tanzania haiwezi kukamilika bila kumtaja Fidel Castro .Hakika kifo chake sio tu ni pigo kwa Cuba bali pia kwa Tanzania na Afrika'',alisema Magufuli.


0 on: " Raisi Magufuli atuma salamu za rambirambi kwa raisi wa Cuba Raul Catsro kufuatia kifo cha Fidel Castro "