Aliyetaka kumuua Tundu Lissu picha yake hii Hapa. Viongozi wa Chadema walitoa tahadhari mapema wakidai kuna mtu aliomba kumuua Tundu Lissu kwa kuandika katika ukurasa wake wa Facebook.
Monday, September 11, 2017

Sababu Zilizofanya Dereva wa Tundu Lissu Asipigwe Risasi Hizi Hapavia to...
12:40 PM
-
No comments
Aliyetaka kumuua Tundu Lissu picha yake hii Hapa. Viongozi wa Chadema walitoa tahadhari mapema wakidai kuna mtu aliomba kumuua Tundu Lissu kwa kuandika katika ukurasa wake wa Facebook.
Friday, September 8, 2017

MBOWE HALI YA TUNDU LISSU NI MBAYA SANA
2:30 PM
-
No comments
Mwanasiasa huyo amekimbizwa hospitali ya mkoa wa Dodoma na kupokea huduma ya kwanza na taarifa zinasema kuna mipango ya kumsafirisha hadi Nairobi kwa matibabu zaidi.
Rais wa Tanzania John Magufuli kupitia kwenye Twitter amesema amesikitishwa sana na kushambuliwa kwa mbunge huyo.
Ameandika: "Nimepokea kwa masikitiko tukio la kupigwa risasi Mh. Tundu Lissu, namuombea kwa Mwenyezi Mungu aweze kupona haraka. Aidha, vyombo vya dola viwasake wale wote waliohusika na tukio hili la kinyama na kuwafikisha ktk mikono ya sheria."
Kwa mujibu wa taarifa ya chama kikuu cha upinzani CHADEMA kwa vyombo vya habari, tukio hilo lilitokea wakati mbunge huyo wa Singida Mashariki akiwa nyumbani kwake.
Thursday, September 7, 2017

Fifa yaamrisha mechi kati ya Afrika Kusini na Senegal kuchezwa tena
8:26 PM
-
No comments
Mechi ya kufuzu kombe la dunia kati ya Afrika Kusini na Senegal itarudiwa tena baada ya refa aliyesimamiwa mechi hiyo kupigwa marufuku na Fifa.
Refa huyo raia wa Ghana Joseph Lamptey, alipiwa marufuku kwa kusimia mechi kwa njia isiyofaa.
Aliwapa penalti Afrika Kusini ambao walishinda kwa mabao 2-1 mwezi Novemba mwaka uliopita kwa kunawa mpira lakini kanda ya video baaadaye ilionyeha kuwa mpira huo ulimgonga kwenye goti mlinzi wa Senegal Kalidou Koulibaly.
Mechi hiyo itachezwa tena Novemba mwaka huu.
Lamptey alipigwa marufuku ya maisha mwezi Machi lakini jana Jumatano marufuku hiyo ilibatiliswa na mahakama ya michezo.
Zaidi Soma BBC Swahili

Mwanasiasa wa upinzani Tanzania Tundu Lissu apigwa risasi na watu wasiojulikana
7:56 PM
-
No comments
Mwanasiasa wa upinzani nchni Tanzania Tundu Lissu amepigwa risasi na watu wasiojulikana jijini Dodoma, katikati mwa Tanzania.
Mwanasiasa huyo amekimbizwa hospitali ya mkoa wa Dodoma na kupokea huduma ya kwanza na taarifa zinasema kuna mipango ya kumsafirisha hadi Nairobi kwa matibabu zaidi.
Rais wa Tanzania John Magufuli kupitia kwenye Twitter amesema amesikitishwa sana na kushambuliwa kwa mbunge huyo.
Ameandika: "Nimepokea kwa masikitiko tukio la kupigwa risasi Mh. Tundu Lissu, namuombea kwa Mwenyezi Mungu aweze kupona haraka. Aidha, vyombo vya dola viwasake wale wote waliohusika na tukio hili la kinyama na kuwafikisha ktk mikono ya sheria."
Kwa mujibu wa taarifa ya chama kikuu cha upinzani CHADEMA kwa vyombo vya habari, tukio hilo lilitokea wakati mbunge huyo wa Singida Mashariki akiwa nyumbani kwake.
Chama hicho kimelaani vikali tukio hilo.
Wakati huo huo, Chama tawala cha CCM, kupitia Katibu wao wa Itikadi na Uenezi,imesema kimepokea kwa mstuko mkubwa kushambuliwa kwa mbunge huyo wa upinzani.
"Chama cha Mapinduzi (CCM) kinalaani tukio hilo la kikatili na lisilo na utu tunalitaka Jeshi la Polisi kuwatafuta, kufanya uchunguzi wa tukio hili na kuchukua hatua kali za kisheria kwa wote waliohusika."
Kamanda wa polisi mkoani Dodoma, Kamishna Msaidizi, Jires Mroto ameiambia BBC kuwa wameanza uchunguzi wa tukio hilo.
"Tunaomba wananchi wenye taarifa ya uhalifu huu, waweze kujitokeza" amesema Kamanda Mroto.
Hivi karibuni, mbunge huyo kutoka chama cha upinzani cha CHADEMA, amekuwa akikamatwa mara kwa mara na polisi akishutumiwa kufanya uchochezi.
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akithibitisha tukio la leo alisema, amesema "yupo hospitali, bado anajaribu kupambana kuokoa maisha yake"
Gazeti la Mwananchi nchini Tanzania, limemnukuu Mganga mkuu wa hospitali ya Dodoma akisema wakili huyo ana majeraha ya risasi miguuni na tumboni.
Saturday, February 11, 2017

Mkalimani akamatwa Tanzania kwa kutafsiri visivyo matamshi ya mtalii
2:08 AM
-
No comments
Mkalimani katika mbuga ya wanyama pori nchini Tanzania amekamatwa baada ya kutafsiri visivyo matamshi ya mtalii mmoja kuhusu nchi na watu wake.
Kwenye video iliyosambazwa kwa wingi, mkalimani huyo anasema kuwa mtalii huyo anataka watu wa Tanzania waache kulalamika kwa sababu ya njaa
Ukweli ni kwamba mwananke huyo anasema kuwa wata wa Tanzania ni wazuri kupindukia.
Alikamatwa siku ya Alhamisi kwa agizo la waziri wa utalii.
Mkalimani huyo ambaye hakutajwa jina ni kutoka mbuga ya Serengeti iliyo kaskazini magharibi mwa nchi.
Kamanda wa polisi eneo hilo Philipo Kalangi, aliiambai BBC kuwa anahojiwa lakini hakutoa habari za kina.
Mwandishi wa BBC mjini Dar es Salaam anasema kuwa huenda waziri alihisi kuwa mkalimani huyo alikuwa akimsuta mtalii au alikuwa akimuiga Rais John Magufuli.
Video hiyo iliyochapishwa na gazeti la Kenya, mtalii anasema:
"Hi. Ziara yangu nchini Tanzania imekuwa nzuri. watu ni wazui na wenye urafiki. Salamu kwa kawaida ni Jambo, nina furaha kuwa hapa, Ardhi ni nzuri."
Mkalimani anatafsiri hivi:
"Anasema watanzania mnalia sana njaa, kila siku mnalia nja wakati mna maua nyumbani, si mchemshe maua mnywe, anasema si vizuri kulia njaa."
Mtalii
"Aina nyingi ya wanyama na watu unaona ni wazuri, kinyume na sehemu zingine. Ni nzuri."
Mkalimani
"Anasema mnamuomba rais wenu awapikie chakula, kwani rais wenu ni mpishi, angahikeni mfanye kazi,chemsheni hata nguo mnywe."
Mtalii
"Ni kitu mabacho utakikumbuka katika maisha yako yote. Ni nzuri na ni ya kupendeza."
Mkalimani
"Anasema mhangaikeni pembezoni za nchi, muache rais hawezi kutoka Ikulu akuje kuwapikia chakula, hivyo mjipikie wenyewe."
Chanzo BBC Swahili
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)