Tume ya umoja wa mataifa kuhusu haki za kibinadam imeonya kuwa mauaji ya kikabila yanaendelea nchini Sudan Kusini.
Tume hiyo iliyoundwa mwezi Machi mwaka huu na yenye wanachama watatu, imekamilisha ziara yake ya siku kumi nchini Sudan Kusini.
Mwenyekiti wa tume hiyo Yasmin Sooka amesema jamii ya kimataifa inastahili kuchuckua hatua za dharura kuzuia mauji ya kimbari kama ilivyotokea nchini Rwanda.
Soma zaidi BBC Swahili
No comments:
Post a Comment